GRACE OF GOD

Image
  THE FOLLOW IS THE STEPS ON HOW  GOD TO HELP YOU Step 1: Be awake to God’s Word to yo Truth:  God’s Word has the answers Read:  “All Scripture is breathed out by God and profitable for teaching, for reproof, for correction, and for training in righteousness, that the man of God may be complete, equipped for every good work” (2 Timothy 3:16-17). Challenge:  Knowing Jesus means knowing what He says. The Bible has everything you need to know about life and godliness. Take some time during the day to read your Bible. The book of John is a good place to start. Start slow, read a few verses and think them over. Look for what God has to say to you, promises he makes, or things He says about himself. Step 2: Be aware of God’s Character Truth:  No matter what, God is good! Read:  “Oh, taste and see that the Lord is good! Blessed is the man who takes refuge in him!” (Psalm 34:8). Challenge:  If God is truly good and love, then take ti...

hongera kwa kuokoka

UTANGULIZI

  
Karibu kwenye Ufalme wa Mungu
Kitabu hiki kimeandikwa kwa ajili yako. Roho Mtakatikfu amekiweka mikononi mwako kwa kusudi muhimu la Mungu ndani ya Kristo.
Katika Jina lile lipitalo majina yote jina la Yesu Kristo, Bwana na Mwokozi wetu, napenda kukukaribisha katika Ufalme wa Mungu!
Imeandikwa wazi kabisa katika kitabu cha Waefeso 2:19 ya kuwa; “Basi tangu sasa ninyi si wageni wala wapitaji, bali ninyi ni wenyeji pamoja na watakatifu, watu wa nyumbani mwake Mungu”.

Umepata neema hii ya Mungu, na sasa umeokoka – biblia inakuambia tangu sasa wewe si mgeni wala mpitaji katika Ufalme wa Mungu - bali wewe ni mwenyeji pamoja na watakatifu wengi waliomo katika nyumba ya Mungu!
Nia ya Roho Mtakatifu kukuwekea kitabu hiki mikononi mwako, ni kukufahamisha angalau kwa kiasi fulani juu ya uamuzi uliofanya wa kutubu dhambi zako, na kumpokea Yesu Kristo kama Bwana na Mwokozi wako.
Kitabu hiki kitakusaidia kujua kitu gani kimetokea ulipookoka na mambo muhimu ya kufanya katika maisha hayo mapya ya wokovu.
Umefanya uamuzi wa busara – katika Luka 15:10 biblia inatuambia ya kuwa hata malaika wa mbinguni wanashangilia na kuufurahia uamuzi huo uliofanya.
Na mimi kama mtumishi wa Mungu aliye hai napenda kumshukuru Mungu katika Kristo Yesu kwa kukufunulia siri hii ya wokovu ambayo wengi hawajaiona na wengine wameiona lakini wanaipuzia. Ni maombi yangu kwa Mungu ya kuwa atakutia nguvu na kukupa ufahamu wa rohoni unapokisoma kitabu hiki ili kikusaidie katika maisha yako ya kila siku.

Comments

Popular posts from this blog

NAMNA YA KUFUNGA ILI UJIBIWE

SOMO: MWONGOZO WA KIBIBLIA WA KUTAFSIRI NA KUOMBEA NDOTO

MADHABAHU. ZA KICHAWI ..KISHETANI~NA ZA KIPEPO ZA VUNJWA KWA DAMU YA YESU